HARMONIZE MATATIZO LYLICS
Haiyee aaah! Olelelelee
Alfajiri imefika Anga inang'aa Mvua inaanza katika Ghafla tumbo la njaa
Naweka sauti kwa spika Nipate umbea wa dar
Mara simu inaita Jina la anko Twaha…Akisema,
Mama yu hoi kitandani Kama si wa leo wa kesho
Na kupona sizani Upate japo neno la mwisho
Mi ndo mtoto wa pekee Nyumbani wananitegemea Mdogo wangu wa kike
Hali duni alishagaolewa
Tizama jasho langu la mnyonge Kipato hakikidhi mahitaji Napiga moyo konde
Yarabi mola ndo mpaji
Matatizo, matatizo Yatakeisha lini Matatizo Kila siku mimi
Ewe mola Matatizo yatakwisha lini Japo likizo Nifurahi na mimi
Mola aliniumba na subira Imani pekee ngao yangu Mbona nishasali sana Ila mambo bado tafarani
Mama kanifunza kikabila Nikonde sana haini yangu Tena nijitume sana Na vya watu nisivitamani
Hata mpenzi niliyenae Najua siku atanikimbia Itanitesa ye ndo nguzo
Zile ngoja kesho badae Atazichoka kuzivumilia Anakosa hata matunzo
Ona, nadaiwa kodi nilipopanga Nashinda road nikihanda Nishapiga hodi kwa waganga
Kwa kuhisi narogwa
Nikauza maji na karanga Nikawa dobi kwa viwanda Ila kote ziro ni majanga
Mtindo mmoja
Mi ndo mtoto wa pekee Nyumbani wananitegemea Mdogo wangu wa kike
Hali duni alishagaolewa
Tizama jasho langu la mnyonge Kipato hakikidhi mahitaji Napiga moyo konde
Yarabi mola ndo mpaji
Matatizo, matatizo Yatakeisha lini (ewe mola) Matatizo Kila siku mimi (jamani matatizo)
Matatizo, (oh matatizo) Yatakeisha lini Japo likizo Nifurahi na mimi (iih matati...)
Matatizo (matati...) Yatakeisha lini Matatizo Kila siku mimi (jama matatizo)
Matatizo, matatizo Yataisha lini (ye iye)
No comments